Monday, May 31, 2010

Mwalimu na mwanafunzi wake

Tembelea http://mawaidha.info

Baada ya kumsomesha muda usiopungua miaka 30, Sheikh alimuuliza mwanafunzi wake:
"Umejifunza nini kutoka kwangu miaka yote hii?"
Mwanafunzi akajibu:
"Kusema kweli sikujifunza isipokuwa machache tu."
Sheikh akasema kwa mshangao:
"Nimekusomesha muda wa miaka 30, kisha unaniambia hukujifunza isipokuwa machache tu! Haya nielezee hayo machache ni yepi?"
Mwanafunzi akasema:
"Niliuangalia ulimwengu, nikaona kila kitu kinmahitajia wa kukiendesha. Kisha nikawaaangalia wanadamu, nikawaona wanawategemea wengine wasiokuwa Mwenyezi Mungu. Na nilipofahamu kutoka kwako ewe ustadhi wangu kuwa hapana kinachoweza kuwepo bila ya Mwenyezi Mungu kutaka, nikaacha kumtegemea ye yote isipokuwa Mwenyezi Mungu."

Sheikh akasema:
"Enhe? Endelea."
Mwanafunzi akasema:
"Kisha nikawaangalia viumbe. Nikaona kila mmoja ana kipenzi chake. Wanaishi pamoja, wanacheza, wanasafiri na kurudi pamoja katika safari zao zote. Lakini katika safari ile ya mwisho, mtu anapowasili kaburini pake, anaingia kule ndani peke yake, na vipenzi vyake vyote vinabaki nje. Hawawezi kumfuata. Nikaona bora nijaalie kipenzi changu kiwe amali zangu njema ili ziwe pamoja nami nitakapokuwa kaburini peke yangu."

Sheikh akasema:
"Ahsante! Ehe? Endelea."
Mwanafunzi akasema:
"Kisha nikawaangalia wanadamu. Nikawaona kila mmoja pesa ikishaingia mkononi mwake haitoki. Watu wake wenye shida hawapati haki zao. Masikini hawapati haki zao. Kisha nikatafakari juu ya maneno ya Mwenyezi Mungu katika Suratul Nahl aya ya 96 isemayo:
مَا عِندَكُمْ يَنفَدُ وَمَا عِندَ اللّهِ بَاقٍ
"Mlivyonavyo vitakwisha na vilivyoko kwa Mwenyezi Mungu (vya jaza yenu) ndivyo vitavyobakia."

Nikawa kila kinachoingia mikononi mwangu hukitoa ili kipate kubaki huko kwa Mwenyezi Mungu."

Kwa kukifafanua zaidi kifungu hiki, tuangalie namna gani Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa Sallam) alivyokuwa akitoa.
Siku moja Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa Sallam) baada ya kuchinja mbuzi na kuigawa nyama yote alimuuliza Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha) kama bado pana chochote kilichosalia. Bibi Aisha akasema:
"Limebaki hili bega tu."
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa Sallam) akamsahihisha kwa kumuambia:
"Bali ile tuliyoigawa ndiyo iliyobaki ewe Aisha."

Katika hadithi nyingine, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa Sallam) amesema:
"Kipo kingine unachofaidika nacho katika mali yako isipokuwa kile unachokula kikaoza tumboni na unachokivaa kikachakaa na unachotoa sadaka kikabaki?"

Sheikh akasema:
"Enhe, endelea."
Mwanafunzi akasema:
"Nikawatizama viumbe. Nikawaona kila mmoja anamuonea husuda mwenzake kwa kile alichokipata. Nikakumbuka maneno ya Mwenyezi Mungu katika Suratul Zukhruf aya ya 32 yasemayo:
أَهُمْ يَقْسِمُونَ رَحْمَةَ رَبِّكَ نَحْنُ قَسَمْنَا بَيْنَهُم مَّعِيشَتَهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَرَفَعْنَا بَعْضَهُمْ فَوْقَ بَعْضٍ دَرَجَاتٍ
"Je, wao wanaigawa rehema ya Mola wako (wakampa wampendae na kumnyima wamtakae?) Sisi tumewagawiya maisha yao katika uhai wa dunia na kuwainua baadhi yao daraja kubwa juu ya wengine."

"Nikaacha kuwahusudu viumbe”.
Sheikh akasema:
"Ahsante. Endelea."
Mwanafunzi akasema:
"Kisha nikawatizama wanadamu. Nikaona tonge imewadhalilisha na kuwafanya wapige mbizi katika mambo ya haramu. Nikakumbuka maneno ya Mwenyezi Mungu katika Surat Hud aya ya 6 ِAliposema:
وَمَا مِن دَآبَّةٍ فِي الأَرْضِ إِلاَّ عَلَى اللّهِ رِزْقُهَا وَيَعْلَمُ مُسْتَقَرَّهَا وَمُسْتَوْدَعَهَا كُلٌّ فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ
"Na hakuna kiumbe cho chote katika ardhi ila riziki yake iko juu ya Mwenyezi Mungu. Na anajua makao yake ya milele na mahali pake pa kupita tu.Yote yamo katika kitabu kinachodhihirisha (kila kitu)."

Nikafahamu kuwa riziki yangu hawezi kuichukua mwengine, na hapo moyo wangu ukatulia. "

Katika kukisherehesha kifungu hiki tuzingatie maneno ya Hassan Al-Basri (Radhiya Llahu anhu) mmoja katika Maulamaa wa At-Tabiina. (waliowaona Masahaba (Radhiya Llahu anhum) lakini hawakumuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa Sallam).
Hassan Al Basri alisema:
"Nilipotambua kuwa amali zangu hawezi kunifanyia mwengine, nikapania kuzifanya mwenyewe. Na nilipotambua kuwa riziki yangu hawezi kuichukuwa mwengine, moyo wangu ukatulia. Na nilipotambua kuwa Mola wangu ananiona, nikaona haya asije akaniona nikiwa katika hali ya kumuasi.”

Wasalaam alaykum wa Rahmatullahi wa Barakatuh

Wabunge watano hoi kura ya maoni


WABUNGE watano na mwakilishi wawili wamebwagwa na hivyo kupoteza nafasi ya kusimama kutetea nafasi zao kwenye uchaguzi mkuu ujao baada ya kumalizika kura za maoni ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), kisiwani Pemba.Wabunge hao wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na mwakilishi mmoja wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar hawatashiriki katika uchaguzi mkuu wa 2010 baada ya kuanguka katika hatua hiyo ya mwanzo kisiwani Pemba ambako CUF ina nguvu kubwa.

Katiba ya CUF imerudisha mamlaka ya kuteua wagombea wa nafasi za ubunge, uwakilishi na udiwani kwa wananchi majimboni mwao ili kuamua nani anawafaa kuwawakilisha katika uchaguzi mkuu.

Habari kutoka kwa makatibu wa CUF wa wilaya na majimbo zinawataja wabunge walioanguka kuwa ni Omar Ali Mzee wa jimbo la Kiwani wilaya ya Mkoani, Juma Said Omar (Mtambwe, Wete), Salim Yussuf Mohammed (Kojani), Mwadini Abbas Jecha (Wete).

Wengine ni Fatma Maghimbi wa Chakechake Wilaya ya Chakechake.

Wawakilishi walioanguka Muhidin Mohamed Muhidin wa Mtambile na mwakilishi wa jimbo la Chambani Wilaya ya Mkoani, Abbas Juma Mhunzi.

Katibu wa Wete, Mkoa wa kaskazini, Maulid Khalid alisema katika jimbo hilo mbunge wa sasa Mwadini Abbass Jecha alimanguka baada ya kuambulia kura 255.

“Mbarouk Salum alishinda katika kura ya maoni ya ubunge wa jimbo la Wete baada ya kupata kura 885 na kuwaangusha wagombea wengine sita,” alisema Khalid.

Wagombea wengine ni Mohammed Khalfan (500), Ali Jabir (300), Kombo Hamis (186), Hamad Issa (110) na Seif Azzan (90).

Kwa upande uwakilishi, Khalid alisema Asaa Othman Hamad ambaye ni mwakilishi wa sasa, alifanikiwa kurudi kwa kupata kura 1,300. Khalid alisema wagombea wengine walioshiriki katika kinyang’anyiro cha kutafuta ridhaa ya chama katika nafasi ya uwakilishi ni Harif Said (407), Maryam Abdallah (397), Issa Rubea (130) na Masoud Hamad (50).

“Kura zote kwa jimbo langu zilikuwa 2,300 na kura 70 ziliharibika,” alisema Khalid.

Katibu wa CUF wa Jimbo la Kojani, Nassor Ali Othman aliliambia Mwananchi jana kwa njia ya simu kuwa Salim Yussuf Mohammed alipoteza nafasi ya kutetea kiti hicho baada ya kuambulia 355 wakati mshindi, Rashid Ali Omar alizoa kura 1,130.

Othmani alisema wagombea wa ubunge katika kura hiyo ya maoni walikuwa Asaa Mkambaya (899), Juma Khamis (437), Ghalib Mohammed (224), Haji Mussa (168), Hamad Bakar (158), Hamad Omar (138), Salim Hamad (71) na Omar Juma kura 38.

“Kura zote kwa upande wa ubunge zilikuwa 3696 wakati kura 77 ziliharibika. Kwa upande wa uwakilishi kura zote zilizopigwa zilikuwa 3,704 lakini kwa bahati mbaya kura 411 ziliharibika,” alisema Othman.

Othman alisema kuwa mwakilishi wa zamani, Omar Ali Jadi alishinda baada ya kupata kura 1,204.

Katika uchaguzi huo uliokuwa na ushindani mkubwa, mwakilishi huyo alimshinda mpinzani wake wa karibu, Hassan Hamad aliyepata 1,192, huku Ali Mjaa Ali akiambulia kura 504 na Salim Bakar Salim (393).

Katibu wa jimbo la Mtambwe, Seif Massoud Sheha aliliambia Mwananchi kuwa mbunge wa sasa, Juma Said Omar aliangushwa na Said Suleiman Said aliyepata kura 693.

“Kwa upande wa ubunge tulikuwa na jumla ya wagombea 12 na uwakilishi wagombea saba. Kura zote kwa ubunge zilikuwa 2,403 lakini kura 47 ziliharibika,” alisema Sheha.

Kwa mujibu wa Sheha, Said Suleiman Said alipata kura 693, Mohammed Hamad Osama' (387), mbunge wa sasa, Juma Said Omar (319) na Salim Sheha (231).

Wengine ni Said Masoud (179), Omar Mbarouk (140), Suleiman Mbarouk (127), Rubea Suleiman (107), Seif Masoud (47), Saleh Ali ambaye alikuwa mbunge wa jimbo hilo mwa 1995-2000 (43), Abdallah Ali (43) na Salim Mussa Mjaka (15).

Kwa upande wa uwakilishi Sheha alisema mwakilishi wa jimbo hilo Salim Abdallah amechaguliwa kutetea nafasi yake baada ya kupata kura 676.

Wagombea wingine ni Ghalib Amour (446), Ali Said (380), Bakar Ali (284), Mohammed Suleiman (284), Saida Khamis (189) na Abbas Ali kura 87.

Kwenye jimbo la Gando, katibu wa CUF, Khelef Mohammed Khelef alisema mbunge wa sasa, Khalifa Suleiman Khalifa amefanikiwa kurudi kwa kupata kura 800.

Kaimu katibu wa Wilaya ya Mkoani, Makame Khalid Makame alisema kuwa hadi sasa ni majimbo matatu tu katika wilaya yake ambayo yamekamilika.

“Katika majimbo hayo mbunge wa Kiwani, Omar Ali Mzee ameanguka huku mwakilishi wake akifanikiwa kurudi; Chambani mwakilishi ameanguka huku mbunge akifanikiwa kurudi; jimbo la Mkanyageni Mohammed Habib Mnyaa na mwakilishi wake wote wamepita,” alisema Makame.

Wabunge na wawakilishi wengi walioanguka hawakuweza kupatikana jana kuzungumzia matokeo ya kura hizo za maoni.

Lakini mbunge wa Kojani, Salim Yussuf alisema: “Aaah nimeyapokea kama yalivyokuja, sina la kuzungumza zaidi. Wakubwa wenyewe wataangalia kwa sababu katiba yetu inasema baraza kuu la uongozi ndio lenye maamuzi ya mwisho.”

“Lakini kilichotokea….aaa…sikelewi lakini ndio kimetokea,” aliongeza Yussuf ambaye pia alikuwa mwakilishi wa jimbo la Pandani kuanzia 1995 hadi 2005..

Mbunge wa Kiwani, Omar Ali Mzee alisema anakubali matokeo kwa kuwa hayo ndiyo maamuzi ya wananchi ingawa uzawa kutoka kijiji kimoja hadi kingine ulichangia sana yeye kuanguka.

“Unajua kura ndio kura, lakini uzawa umechangia sana mimi kuanguka. Kwa sababu kila kijiji kilitaka mgombea atoke kwao kwa hiyo kura zikagawika sana. Mathalani vijiji vya Kiwani, Kendwa, Mwambe, Chwaka, Nanguji, Mwambe na Mtangani vyote vilikuwa na wagombea,” alisema Mzee.

Kura zinaendelea kupigwa kisiwani humo huku nyingine zikiendelea kuhesabiwa.
SOURCE: MWANANCHI

Waliopata vitambulisho vya ukaazi washindwa kujiandikisha DKWK Z`bar


Wanzanzibari 99,047 waliopata vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi, hawajajitokeza kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (DKWK) visiwani hapa.

Mkurugenzi wa idara ya usajili wa vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi, Mohammed Juma Ame, alisema hayo wakati akizungumza na Jukwaa la Wahariri mjini hapa mwishoni mwa wiki.

Alisema kwa mujibu wa takwimu zilizopo, jumla wa watu 408,178 wamesajiliwa katika DKWK ilipofika Mei 9, mwaka huu.

Aidha, alisema Wazanzibari 562,008 wameshapewa vitambulisho hivyo tangu usajili huo ulipoanza mwaka 2005.

Ame alisema kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec), idadi ya watu waliotarajiwa kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ni 500,000.

Ame alisema ipo haja yakufanya utafiti ili kujua sababu za watu waliopata vitambulisho vya kudumu, kutojiandikisha kwa ajili ya kupiga kura.

“Idadi ya watu waliopata vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi, wakashindwa kujiorodhesha kwa ajili ya kupiga kura ni kubwa, haiwezekani wawe wamehama Zanzibar au kufa,” alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo, kuna haja kwa taasisi zinazohusika kufanya utafiti wa kina ili kubaini sababu zake.

Hata hivyo alisema Wazanzibari wengi wameanza kuchoshwa na ahadi za wanasiasa, na kuamua kutojiakishaji kupiga kura.

“Zanzibar watu wameanza kuchoshwa na ahadi za wanasiasa na kuamua kutojitokeza kuandikishwa kuwa wapiga kura, licha ya kwamba wana vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi,” alisema.

Hata hivyo, alisema uchunguzi walioufanya ulibaini kuwa baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa (masheha) wanajihusisha na urasimu katika utoaji wa fomu za kuwawezesha kupata vitambulisho.

Alisema urasimu huo unafanyika kwa visingizio vya kuishiwa fomu, na wengine (masheha) wanatoza fedha ili kutoa barua za usajili.

Ame alisema idara yake imeanza kuwaorodhesha masheha wenye tabia hiyo, ili waweze kuchukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria.

Alisema kuanzia Desemba, 2009 hadi Mei mwaka huu, ofisi ya usajili wa vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi, ilipokea rufaa 515, 405 kati ya hizo zilitoka Unguja wakati 110 zilitoka Pemba. Zote zimefanyiwa kazi.

Hata hivyo alisema kwamba idadi kubwa ya rufaa za Pemba zilionyesha kuwa wahusika walishindwa kupata vitambulisho kutokana na kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa.

Alisema wengi wao walionyesha kadi za kliniki badala ya cheti kama inavyotakiwa kwa mujibu wa sheria.

Mkurugenzi huyu alisema Machi 23, mwaka huu, Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad, aliwasilisha malalamiko mapya kwa Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, na kukabidhi orodha ya watu 3,235 waliodai kunyimwa vitambulisho, lakini baada ya uchunguzi, madai hayo yalionekana si ya kweli.

Hata hivyo alisema baada ya orodha hiyo kuhakikiwa, ilibainika kuwa watu 2,018 wamesajiliwa tangu 2005, lakini wameshindwa kuchukua vitambulisho vyao katika ofisi za usajili za wilaya zilizopo Unguja na Pemba.

CHANZO: NIPASHE

Friday, May 28, 2010

BREAKING NEWSS....Lahore mosques attacked, 30 feared killed


Heavily armed terrorists on Friday stormed two packed mosques of the minority Ahmadi sect in Lahore on Friday, firing indiscriminately with automatic weapons and lobbing grenades.
At least 30 people are feared killed in the apparently coordinated attacks by two groups of terrorists, who stormed into the mosques at around 1.45 pm local time. The terrorists targeted the mosques in Garhi Shahu and Model Town areas of Lahore.
Witnesses said two groups of attackers lobbed grenades and fired as they entered the mosques. Police and paramilitary forces surrounded the two mosques and took up positions on roads and roof tops around the mosques.
Geo News channel reported that a Punjabi wing of Tehrik-e-Taliban Pakistan claimed responsibility for the attacks.
The channel also reported that there were over 1,500 worshippers in the sprawling mosque complex at Model Town but this could not be officially confirmed. Reports said the firing was still continuing at both the sites.
IANS reports a Taliban group has claimed responsibility for the attack.
Suicide bombers struck at a market in Lahore city March 12, killing 45 and injuring over 100.
Pakistan has seen scores of attacks by groups of Islamist militants against government, Western and security force targets over the past three years. Lahore, the second largest city in the country and a vital a military and political centre, has been the scene of several.
Many Islamist militants believe it is permissible or honourable to kill non-Muslims, or even those Muslims who do not share their extreme views.
The Ahmadis call themselves Muslims but believe their founder declared himself a prophet centuries after Muhammad, who other Muslims believe was the final prophet. They have long been subject to informal and state-sanctioned discrimination in Pakistan.
The government has declared them a non-Muslim minority and they are prohibited from calling themselves Muslims or engaging in Muslim practices such as reciting Islamic prayers..